Kitabu hiki kinamwelekeza mwanafunzi katika uandishi wa insha mbalimbali. Wanafunzi wengi pamoja na walimu hukwepa kipengele cha insha kwa madai kuwa hakivutii; jambo ambalo linasababisha matokeo mabaya. Kutokana na haya, kitabu hiki kinatoa maelekezo kwa wanafunzi na walimu kuhusu ufundishaji wa insha kwa njia bora zaidi.